У вашего броузера проблема в совместимости с HTML5
Kulitokea kizaazaaa katika mji wa Embu, baada ya mwanamke mmoja kumfumania mumewe akila uroda na mwanamke mwingine kwenye vyumba vya kulala, huku akimfungia mwanawe mwenye umri wa miaka 2 kwenye chumba hicho. Mwanamume huyo anasemekana kuondoka nyumbani jana saa nne usiku na mwanawe aliyekuwa akiugua , na alisema kuwa anampeleka hospitalini, lakini hakurejea nyumbani, na mkewe akamfumania na mwanamke mwingine kwenye nyumba hiyo ya malazi.