Saturday, 20 September, 2025г.
russian english deutsch french spanish portuguese czech greek georgian chinese japanese korean indonesian turkish thai uzbek

пример: покупка автомобиля в Запорожье

 

Mikanda Ya Ubingwa Wa Global Tv Hadharani

Mikanda Ya Ubingwa Wa Global Tv HadharaniУ вашего броузера проблема в совместимости с HTML5
KAMISHENI ya Ngumi za Kulipwa Tanza­nia (TPBO) imeiweka hadharani mikanda itakayogombaniwa katika mapambano ya Tubing wa Global TV, Afrika Mashariki na Kati yatakayofanyika Julai 22, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Dar Live, Mbagala Zakhem, Dar. Katika mapambano hayo ya kimataifa yat­akayorushwa mubashara na Kituo cha Global TV Online kupitia webiste yake ya www.globaltvtz. com, Bondia wa Tanzania, Francis Miyeyusho ‘Chichi Mawe’ atapambana na Is­rael Kamwamba wa Ma­lawi. Pambano lingine litakuwa ni kati ya Idd Pi­alali dhidi ya Regin Cham­pion raia wa DR Congo, wakati Nasibu Ramadhan ‘Pacman’ atacheza na Ti­nashe Mwadziwana kuto­ka Zimbabwe. Mapamba­no hayo yote ni ya raundi kumi. Rais wa TPBO, Yassin Abdallah ‘Ustaadh’, amei­tambulisha mikanda itakayogombaniwa katika mapambano hayo huku akithibitisha uwepo wa Balozi wa Malawi wa hapa nchini, Hawa Ndilowe kwenye pambano hilo. “Maandalizi ya mapam­bano ya kimataifa, kati ya mabondia wa kutoka DR Congo, Malawi na Zim­babwe ambao watapi­gana na mabondia wetu hapa, yamekamilika. Kila kitu kimeshakuwa sawa na wameshapata barua maalum kutoka katika mashirikisho ya nchi zao. “Huo ndiyo mfumo wa ngumi za kulipwa unavy­okuwa, bondia anatakiwa apate ridhaa na kibali cha kwenda kupigana nje ya nchi kutoka kwa kamish­eni, chama au shirikisho la ngumi za kulipwa ndani ya nchi yake.
Мой аккаунт